Nicki Minaj
ameweka headlines kwenye kurasa za burudani kwa siku tatu mfululizo
baada ya kutangaza kuwa ana mimba ya superstaa boyfriend wake Meek Mill, taarifa ambayo imewaweka mashabiki wengi roho juu baadhi wakifurahia na wengine wakiwaza kama ni kweli ana mimba.
Kwenye tour ya mji wa mwisho waliotembelea wiki iliyopita Nicki Minaj alisikika akitoa pongezi za sifa kwa Meek Mill huku akiwaomba mashabiki wampigie kelele za kutosha “baba wa mtoto wake”… so hii ishu ni kweli ana mimba ama anatania tu?
Licha ya hayo Meek Mill ameshasikika kwenye interviews zaidi ya moja akisema kuwa anatamani sana kuwa na mtoto na Nicki lakini ikiwa tu wakiwa ndani ya ndoa. Je msimamo sasa hivi umebadilika?
Mashabiki wana maswali mengi sana, na kama wewe ni miongoni mwa mashabiki wa Nicki Minaj utakuwa umejiuliza maswali mengi sana pia juu ya hii ishu…Hapa chini nimekusogezea kipande cha video na baadhi ya tweets za Nicki za Twitter.
Post a Comment